Tuesday, March 24, 2015

Anonymous

RAIS JK: POLISI MJIANDAE KUKABILIANA NA VURUGU ZA UCHAGUZI

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete akikagua Gwaride la Jeshi la Polisi.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete amelitaka Jeshi la Polisi nchini Tanzania kujiandaa kikamilifu ili kukabiliana na vurugu zozote zitakazojitokeza wakati wa uandikishaji wapigakura, upigaji Kura ya Maoni ya kupitisha Katiba Inayopendekezwa na Uchaguzi Mkuu wa Oktoba, mwaka huu. 

Akifunga mafunzo ya maofisa warakibu wasaidizi katika Chuo cha Taaluma ya Polisi, Dar es Salaam jana, Rais Kikwete alisema dalili zinaonyesha kwamba kuna watu wenye nia ya kuhatarisha amani katika matukio hayo. 


Alisema Serikali itahakikisha kazi ya uandikishaji katika daftari la wapigakura, upigaji wa kura ya maoni na uchaguzi mkuu vinafanyika kwa amani na utulivu kwa gharama zozote. 


Akikuzungumza katika hafla hiyo, Rais Kikwete alisema kama serikali inatambua changamoto zinazolikabili Jeshi la Polisi hasa katika majukumu yake ya kuhakikisha ulinzi wa raia na mali zake, lakini kazi nzito ikiwa ni wakati huu ambapo Taifa linaelekea kwenye upigaji wa kura ya maoni kuhusu katiba inayopendekezwa na uchaguzi mkuu wa Madiwani, Wabunge na Raisi hivyo kulitaka Jeshi la Polisi kutotumia 'maguvu' ili kuifanya amani iendelee kutawala katika kipindi hiki cha uchaguzi. 


Aidha Mwenyekiti wa CUF, Profesa Ibrahim Lipumba Akizungumzia ya Rais Kikwete, alisema, “Rais Kikwete yeye ndiye mtu wa kwanza kuivuruga amani kwa kutangaza tarehe ya kufanyika kwa kura ya maoni wakati siyo jukumu lake na jukumu hilo ni la Tume ya Taifa ya Uchaguzi "NEC" na serikali yake kushindwa kuratibu vyema mchakato wa uandikishaji. 


Profesa Lipumba amesema, na hapa tunamnukuu: "Kama uandikishaji hauendi vizuri mpaka sasa, anavunja sheria za nchi, halafu yeye mwenyewe tena anakwenda kwenye vyombo vya dola na kuvieleza vijiandae, wakati yeye huyohuyo ndiye ameanzisha uvunjifu wa amani tunashindwa tumueleweje,” mwisho wa kunukuu.
CHANZO: IRAN SWAHILI PICHA NA MTANDAO

USIPITWE! JIUNGE NASI FACEBOOK

Subscribe to this Blog via Email :

TOA MAONI YAKO HAPA (MATUSI HAYARUHUSIWI)

Note: Only a member of this blog may post a comment.