Tuesday, March 24, 2015

Anonymous

NEW UPDATES: Kuanguka ukuta wa nyumba ya Diamond, Meneja wake na Mkandarasi wafunguka kihivi #UHeard

Kutokana na mvua kubwa zilizonyesha DAR na kuleta maafa ya mafuriko kwa baadhi ya sehemu, nyumba ya kifahari ya msanii Diamond Platnumz ambayo  ujenzi wake haujakamilika nayo imekumbwa na madhara ya mvua baada ya ukuta wake kuanguka.

Mtaalam wa majengo fundi Saidi amesema tukio kama hilo linaweza kutokea kutokana ukuta kutowekwa zege la kutosha chini, na juu inawezekana hapakufungwa mkanda. 
Soudy Brown alimtafuta Diamond lakini hakuweza kumpata kwenye simu kwa muda mrefu, akamtafuta meneja wake ambaye ni Said Fella. 

Fella amesema ni kweli ukuta wa nyumba hiyo umeanguka kutokana na mvua zinazoendelea kunyesha lakini bado iko chini ya mkandarasi na anatakiwa kukabidhi mwezi wa sita kwa hiyo kuhusu suala la ukarabati liko mikononi mwao.

Ili kusikiliza story yote bonyeza play hapa chini…

USIPITWE! JIUNGE NASI FACEBOOK

Subscribe to this Blog via Email :

TOA MAONI YAKO HAPA (MATUSI HAYARUHUSIWI)

Note: Only a member of this blog may post a comment.