Tuesday, March 17, 2015

Anonymous

Hii style aliyotumia kuutoa ujauzito wa mpenzi wake ni ishu ambayo imechukua headlines duniani!


woman-holding-cocktail-glass-bar
Mwanaume mmoja Norway anashikiliwa kwa tuhuma za kumsababishia majeraha mpenzi wake pamoja na kumtoa ujauzito bila ridhaa yake, baada ya kumuwekea vidonge kwenye kinywaji na kusababisha ujauzito wake kuharibika. 

Jamaa huyo alifanya ukatili huo baada ya kumuwekea mpenzi wake vidonge ya kutoa mimba kwenye kinywaji alichokuwa anakunywa kwa lengo la kumtoa ujauzito wa miezi minne aliokuwa nao, ambapo alifikia hatua hiyo baada ya kumshawishi kuutoa kwa muda mrefu bila mafanikio. 

Mwanamke huyo amesema mpenzi wake alikuwa akimshawishi mara nyingi kutoa ujauzito huo lakini hakukubaliana nae, baada ya kunywa kinyaji hicho alisikia maumivu makali ya tumbo na ujauzito wake kutoka, alipoenda Hospitali na kufanya vipimo ilionekana ujauzito wake umeharibika tayari. 

Hata hivyo mtuhumiwa huyo alikiri kufanya kosa hilo na kusema anajisikia vibaya ila amefanya hivyo kwa sababu ilikuwa njia pekee ya kufanikisha lengo lake kuutoa ujauzito huo, Mahakama imemhukumu kifungo cha miaka saba jela.

USIPITWE! JIUNGE NASI FACEBOOK

Subscribe to this Blog via Email :

TOA MAONI YAKO HAPA (MATUSI HAYARUHUSIWI)

Note: Only a member of this blog may post a comment.