Tunafahamu
kuwa ndege hulazimika kutua gafla ikiwa katika safari yake pale tu
ambapo kunatokea hitilafu ikiwa angani na kusababisha kutua hata kama
haijamaliza safari yake.
Unaweza
ukadhani si jambo rahisi lakini hii ni ya kweli imetokea baada ya ndege
moja ya shirika la ndege la British Airways kulazimika kutua kufuatia
harufu mbaya iliyokuwa ikitokea ndani ya choo.
Ndege hiyo ilikuwa ikielekea Heathrow Uingereza kutoka Dubai safari ambayo kwa kawaida huchukua saa saba.
Abiria mmoja aliyekuwa ndani ya ndege hiyo Abhishek Sachdev,
aliandika kwenye mtandao wake wa kijamii wa Twitter kuwa ”ndege yetu ya
British Airways imelazimika kurejea dubai baada ya wahudumu kugundua
kuwa harufu mbaya inatokea kwenye choo cha ndege hiyo.”
Rubani wa ndege hiyo alimwita msimamizi
wa wahudumu wa ndege hiyo ndipo wakagundua kulikuwa na harufu mbaya ya
choo katika safari yao iliyotokea ndani ambayo inaweza kuhatarisha afya
zao.
Alisema ilikuwa ni tayari nusu saa tangu
waanze safari na kulazimika kurejea Dubai na hakukua na ndege mbadala
ya kuwarejesha London hivyo kusubiri kwa zaidi ya saa 15 .

Note: Only a member of this blog may post a comment.