Mrembo na staa wa Bongo Movies, Rose Ndauka siku ya jana akiwa paomja
na team yake ya Rozzie ambao ni watoaji wa jarida la kila wiki la
Rozzie walitembelea kituo kimoja cha kulelea watoto wenye changamoto
mbali mbali hapa jiji Dar es salaam, mbali na kutoa msaada mbali mbali,
Rose na team yake walishiriki michezo mbali mbali na watoto hao.
“Si kitu kibaya kutenga muda wa kuwafariji wenzetu wenye matatizo,
Jumapili ya jana ilikuwa nzuri sana kwa upande wetu tuliweza kuwakilisha
vizuri tu na kucheza michezo mingi na watoto”-Rose aliandika mtandaoni

Hapo juu ni baadhi ya picha ya tukio hilo.
Hongera sana Rose na team yako, muendelee kuwa na moyo huo ili kuonyesha njia kwa wengine.
-bongomovies
-bongomovies

Note: Only a member of this blog may post a comment.