Katika interview mbili nimewahi kumsikia Diamond Platnumz akitoa
msemo mmoja unaofanana lakini katika hizo interview mbili tofauti,
akitabasamu alisema ‘kama nafanya kazi kwa bidii ni lazima niishi vizuri
pia, nipate ninavyotaka’
Kwa hii picha ya gari aliyopost Diamond kwenye instagram labda ndio
anaendelea kutimiza ndoto zake? Japokua hakuandika chochote baada ya
kuiweka picha hii ya gari jipya lisilo na namba, baadhi ya mashabiki
wameanza kumpongeza ila bado tunaendelea kumtafuta ili
tupate uhakika kama ndio mkoko wake mpya.
JIUNGE NASI FACEBOOK > >>BONYEZA HAPA.
KAMA KUNA TATIZO AU UNA PICHA ZA MATUKIO TUTUMIE WHATSAPP +255 712 919 142.
ASANTE NA KARIBU TENA!
-via millardayo



Note: Only a member of this blog may post a comment.