Lungi: Nina mpenzi wangu ambaye nampenda sana na naamini bila yeye maisha yangu hayajakamilika.
Ijumaa: Hivi siku ukimfuma huyo mpenzi wako na mwanamke mwingine utajisikiaje na utachukua hatua gani?
Ijumaa: Mastaa mnatisha kwa kuchuna mabwana, wewe vipi ulishawahi kupitia maisha hayo ya kuchuna mabuzi?
Lungi: Nimeshawachuna sana kwani wamekuwa wakinifuata wao, si unajua nilivyo mrembo na shepu ninayo ndiyo wanachanganyikiwa kabisa.
Ijumaa: Kwa hiyo umeshatembea na wanaume wengi kwa sababu ya pesa, si ndiyo?
Lungi: Mimi mjanja bwana, wengine naishia kuwachuna tu lakini hawaoni ndani.
Ijumaa: Hivi mtu akikuuliza ni kazi gani inakuweka mjini utamjibuje? Maana unaonekana upoupo tu.
Lungi: Mimi ni mfanyabiashara, huwa nakwenda Sauzi, China na Dubai kwa ajili ya kuleta nguo na vitu vya wanawake.
Ijumaa: Wafanyabiashara wengi hasa wanaokwenda nchi hizo ulizotaja wanadaiwa kufanya biashara ya ‘sembe’. Wewe ushawahi kubeba mzigo?
Lungi: Ukweli nimewahi kubeba unga na kuwa mfanyabiashara mzuri tu lakini nimeacha kwani niligundua ni biashara mbaya sana na naomba Mungu anisamehe.
Ijumaa: Nani alikushawishi kuingia katika biashara hiyo mbaya?
Lungi: Ni rafiki yangu mmoja hivi ila siwezi kumtaja, najuta na sitarudia tena.
Ijumaa: Kwa kufanya biashara hiyo ulinufaikaje na unawashauri nini wale wanaotamani kufanya kazi hiyo wakiamini watapata mafanikio ya haraka?
Lungi: Kimsingi sijafaidika sana, ni kazi hatari ambayo simshauri mtu kuifanya. Si wanasikia yanayowakuta watu wanaogeuzwa punda?
Ijumaa: Ushawahi kutoa mimba?
Lungi: Sijawahi, mimi naona ni uuaji.
Ijumaa: Unatajwa kuwa mmoja wa mastaa wenye tabia ya kuwaunganisha wenzako kwa wanaume, hili nalo likoje?
Lungi: Ilikuwa zamani lakini sasa nimeacha, nimeona ni kazi isiyo na manufaa kwangu.
INAUMA SANA: BAADA YA KUGEUZWA KICHAKA CHA UFUSKA, OFISI YA KANUMBA YAFUNGWA RASMI!
===>>SOMA ZAIDI HAPA!
===>>SOMA ZAIDI HAPA!
JIUNGE
NASI FACEBOOK > >>BONYEZA HAPA.KAMA KUNA TATIZO AU
UNA PICHA ZA MATUKIO TUTUMIE WHATSAPP +255 712 919 142.ASANTE NA KARIBU
TENA!


Note: Only a member of this blog may post a comment.