Monday, February 9, 2015

Anonymous

INAUMA SANA: WASTARA AWACHARUKIA WANAOMTUSI MUMEWE!

Stori Na:Gladness Mallya/Ijumaa Wikienda 
MSANII mkongwe katika gemu la filamu Bongo, Wastara Juma ameapa kumshtaki mtu atakayekamata kutokana na baadhi ya mashabiki kuwa na tabia ya kumtukana matusi ya nguoni mtandaoni huku wakimhusisha na marehemu mumewe, Sajuki. 
Msanii mkongwe katika gemu la filamu Bongo, Wastara Juma.
Akizungumza na gazeti hili, Wastara alisema anajisikia vibaya baadhi ya mashabiki wanavyomtukana kwenye mitandao ya kijamii jambo ambalo siyo zuri kwani wanaingilia maisha yake binafsi na kibaya zaidi wanamhusisha Sajuki. 

“Ukweli sipendi kabisa na nitamshtaki mtu maana wananitengenezea chuki kwani wakati mwingine wananitukana, wanamtukana sana Bondi huku wakidai kwamba nilikuwa naomba Sajuki afe ndiyo nifanye mabaya sasa sijui nimefanya kitu gani kibaya, kuwa na Bondi nimekuwa naye baada ya mume wangu kufariki maana mimi ni binadamu na kama angekuwepo nisingekuwa na mwanaume mwingine zaidi yake,” alisema Wastara.
JIUNGE NASI FACEBOOK > >>BONYEZA HAPA.KAMA KUNA TATIZO AU UNA PICHA ZA MATUKIO TUTUMIE WHATSAPP +255 712 919 142.ASANTE NA KARIBU TENA!

USIPITWE! JIUNGE NASI FACEBOOK

Subscribe to this Blog via Email :

TOA MAONI YAKO HAPA (MATUSI HAYARUHUSIWI)

Note: Only a member of this blog may post a comment.