Friday, December 23, 2016

Unknown

Marekani si sehemu rahisi kuishi kwa mtu mweusi – Abela (The Amazing)

Mwanamuziki wa kundi la The Amazing, Abela, amesema Marekani ni nchi yenye changamoto nyingi kuishi kwa mtu mweusi.

Ameiambia Bongo5 kuwa hiyo ni sababu kubwa iliyomfanya aamue kuja kuishi Tanzania kwakuwa maisha ya huku ni ya upendo na kuheshimiana zaidi.
“Marekani si sehemu rahisi kwa kuishi,” anasema. “Sasa hivi kuna uhasama mkubwa wa rangi Marekani, hivyo kuwa mtu mwenye rangi ni ngumu kiasi.Nina furaha kuwa nyumbani kwenye sehemu ambayo kila mtu anaelewena na mwenzie na ni nchi yenye amani,” ameongeza.

Abela anasema hata hivyo haikuwa rahisi tu kuamua kuondoka Minnesota ambako wazazi wake wanaishi kuja Dar. “Haikuwa rahisi, na ni ngumu kidogo kuwashawishi watu kwamba muziki unaweza kuwa kazi,” anaeleza.
“Kwahiyo nimekuja hapa kivyangu na nilijiamini mwenyewe, ninafurahi kuwa nilichukua uamuazi huo, haikuwa rahisi lakini ninaona matokeo, bila shaka inalipa.”

Anasema familia yake inamuunga mkono kwakuwa baba yake pia ni mtengezaji wa filamu hivyo naye ni msanii. Ameongeza kuwa wameshangaa pia kuona kile anachokifanya kimeanza kuzaa matunda tayari.  -via Bongo5

USIPITWE! JIUNGE NASI FACEBOOK

Subscribe to this Blog via Email :

TOA MAONI YAKO HAPA (MATUSI HAYARUHUSIWI)

Note: Only a member of this blog may post a comment.