Tuesday, September 13, 2016

Unknown

BARNABA Awataka Wasanii Kuwekeza Nguvu Nyingi Kwenye Kuandaa Audio Na Sio Video

Msanii na mtayarishaji wa muziki kutoka ‘High Tible Sound’ Barnaba Classics amewataka wasanii wenzake kuwekeza nguvu nyingi kwenye kuandaa audio za nyimbo zao. 

Akiongea na Bongo5 Jumapili hii, Barnaba amesema wasanii wanajikuta wanaweka nguvu kubwa kwenye kuandaa video kubwa kuliko audio hali ambayo amedai inashusha muziki wa Tanzania.

“Asikudanye mtu muziki mzuri unapatikana kwenye audio nzuri,” alisema Barnaba. “Ukifanikiwa kuandaa audio kali sasa ndo ufikirie issue ya video,lakini unakuta wasanii sasa hivi wanatumia nguvu kubwa kuandaa video kuliko audio, mimi nataka kuwaambia kitu kikubwa kwenye muziki ni audio, mengine baadae,”

Muimbaji huyo ambaye ameachia video ya wimbo ‘Lover Boy’ hivi karibuni amewataka wasanii kuwekeza nguvu nyingi kwenye audio kuliko kwenye video.

-via Bongo5

USIPITWE! JIUNGE NASI FACEBOOK

Subscribe to this Blog via Email :

TOA MAONI YAKO HAPA (MATUSI HAYARUHUSIWI)

Note: Only a member of this blog may post a comment.