Monday, May 16, 2016

Anonymous

Msanii Huyu wa Komedi Afunga Ndoa Kimya Kimya [ +PICHAZ ]

Msanii wa vichekesho, Mkono Mkonole, Jumamosi hii amefunga ndoa kimya kimya mkoani Tanga na mwanadada aitwae Sabrina Ally.
Akiongea na Bongo5 Jumatatu hii, Mkono amesema amefunga ndoa kimya kimya kutokana na kifo cha msanii mwenzake, Kinyambe aliyefariki Mkoani Mbeya wiki iliyopita na kuzikwa huko huko.
“Nimefunga ndoa jumamosi hii mkoani Tanga, sema ndoa ilikuwa kimya kimya kutokana na msiba wa msanii mwenzetu Kinyambe, lakini nashukuru mungu kila kitu kimeenda sawa,” alisema Mkonole.
Pia Mkonole amesema ameamua kuoa mke ambaye anatoka nje ya tasnia yake ya filamu kwa madai wanawake wa kwenye tasnia hiyo ni wajanja wajanja.
13179318_1076811212391304_4238589915757276506_n
13230112_224611137921535_7171777436986899601_n
13237742_224610931254889_1994034079809088419_n 
-via Bongo5

USIPITWE! JIUNGE NASI FACEBOOK

Subscribe to this Blog via Email :

TOA MAONI YAKO HAPA (MATUSI HAYARUHUSIWI)

Note: Only a member of this blog may post a comment.