Tuesday, April 12, 2016

Anonymous

Kundi la Mziki la Navy Kenzo Wala Shavu la Ubalozi Airtel Tanzania


Uwekezaji wao sasa umeanza kulipa. Kundi la Navy Kenzo limepata shavu la ubalozi wa promotion mpya ya Airtel.
Kundi hilo linaloundwa na Nahreel na mchumba wake Aika litakuwa balozi wa promotion ya Jipimie Airtel Yatosha.

“Tunapenda kuwataarifu rasmi kama Navy Kenzo ni Ambassador wapya wa #JipimieAirtelYatosha ambayo ni bundle mpya na za kipekee wewe kama mteja unaweza kujipimia chochote utakacho iwe dakika, sms au Mb pekee au vyote tu piga *149*98# #jipimieyatosha,” wameandika kwenye Instagram.
Navy Kenzo wamejipatia umaarufu Afrika kwa ngoma zao, Game na Kamatia zenye video kubwa na za gharama.

USIPITWE! JIUNGE NASI FACEBOOK

Subscribe to this Blog via Email :

TOA MAONI YAKO HAPA (MATUSI HAYARUHUSIWI)

Note: Only a member of this blog may post a comment.