Thursday, April 7, 2016

Anonymous

DAYNA Nyange Awachana Mashabiki

Mwanaisha Said ‘Dayna Nyange’
Boniphace Ngumije
Staa wa Ngoma ya Angejua, Mwanaisha Said ‘Dayna Nyange’ amewatolea uvivu watu wanaofuatilia maisha yake katika mitandao ya kijamii kuwa hakuna anayemsaidia kuyaendesha.
Akichonga na Showbiz, Dayna aliyewahi pia kubamba na ngoma kadhaa kama vile Mafungu ya Nyanya alisema kuwa, suala la kuwa na skendo kwa msanii ni jambo la kawaida hivyo anawashangaa wanaoendelea kumuandama kila kukicha kutokana na skendo anazokumbana nazo.
“Huwa inanikera sana kuona watu wananiandama bila mpango wakati hakuna anayenisaidia kuendesha maisha yangu, niachwe huru maana hata hizo skendo wao haziwahusu,” alisema Dyna.

USIPITWE! JIUNGE NASI FACEBOOK

Subscribe to this Blog via Email :

TOA MAONI YAKO HAPA (MATUSI HAYARUHUSIWI)

Note: Only a member of this blog may post a comment.