Andrew Carlos
BAADA ya kufanya poa Ngoma ya My Life,
staa wa Muziki wa Bongo Fleva, Abdulaziz Chende ‘Dogo Janja’ amefunguka
kuwa prodyuza aliyemtengenezea ngoma hiyo ambaye ni raia kutoka Norway,
Carl Hovind anahusika pia katika ngoma yake ya pili.
Akichonga na Showbiz Dogo Janja alisema kuwa, Ngoma ya My Life video yake inatarajiwa kuachiwa siku yoyote kuanzia leo na kwamba mashabiki wajiandae kumsikia katika ngoma nyingine iliyopikwa na Carl.
Akichonga na Showbiz Dogo Janja alisema kuwa, Ngoma ya My Life video yake inatarajiwa kuachiwa siku yoyote kuanzia leo na kwamba mashabiki wajiandae kumsikia katika ngoma nyingine iliyopikwa na Carl.
“Video ya My Life ipo tayari
imetayarishwa na Hanscana na inatarajiwa kuachiwa muda na siku yoyote,
nimpe tano za kutosha prodyuza aliyeipika ngoma hiyo, Carl Hovind anajua
ndiyo maana amenitengenezea tena ngoma nyingine ambayo jina lake
litakuwa sapraizi kwa mashabiki,” alisema Dogo Janja.
Note: Only a member of this blog may post a comment.