Video kuchezwa MTV Base au Trace TV bado sio kitu cha kuchukulia poa hasa kama wewe ni msanii wa Tanzania.
Darassa amefanikiwa kwa mara ya kwanza kuwa na video inayochezwa
kwenye kituo cha runinga cha Trace Urban. Video ya wimbo wake ‘Kama
Utanipenda’ akiwa na Rich Mavoko inachezwa kwenye kituo hicho.
Hanscana aliyeongoza video hiyo, amepost picha Instagram inayoonesha video hiyo ikichezwa na kuandika, “s/o
to @tracenigeria to premiere #kamautanipenda kwa upande wa tv za
kimataifa thank you so much @tracenigeria . Na ntazidi kukaza mpaka
mwisho tutakutana tu huko huko . @darassacmg ft @richmavoko
#kama_utanipenda #kamautanipenda.”
Trace ni miongoni mwa vituo vya TV za Afrika vinavyooheshimika zaidi.
-via Bongo5
Note: Only a member of this blog may post a comment.