Mchezaji wa timu ya Manchester United, Juan Mata ameomba radhi
mashabiki wa timu hiyo baada ya kupata kadi nyekundu kwenye mechi yao
dhidi ya West Bromwich Albion.
Mata amepost kwenye akaunti yake ya twitter kwa kusema, baada ya
takribani mechi 500, nimetolewa nje ya uwanja kwa ma ya kwanza. Kwenye
mchezo huu United walifungwa goli moja kwa bila na West Bromwich Albion,
goli ambalo lilifungwa na Rondon dakika ya 66.
Mata amesema, “Baada ya mechi takribani 500 kama mchezaji
professional, kwa mara ya kwanza nimetolewa nje. Hili ni jipya kwangu
lakini tumejifunza. Nimewaumiza sana wachezaji wangu wamecheza wakiwa
kumi kwa muda mrefu.”
“Naangalia mechi inayofuata kwa sasa kwenye Europa League dhidi
Liverpool. Baada ya kufunga goli pekee dhidi ya Watford nimeongeza
uzoefu zaidi,” ameongezea Mata.
Note: Only a member of this blog may post a comment.