Juzi kati msanii wa bongofleva Dogo Janja
alijikuta kwenye vichwa vya habari baada ya kuvujishwa kwa sauti yake
kwenye maongezi ya kumtongoza msichana kwenye simu ambapo akajikuta
ameilalamikia Tiptop Connection kwa kuchelewa kuachia nyimbo zake mpya ili kuuvunja ukimya wa zaidi ya miaka miwili.
Kwenye hayo maongezi ya simu Dogo Janja alijikuta ametoa matusi kwa Tiptop na
alikua huru kuongea mambo mengi sababu alijua ni maongezi ya kawaida ya
simu na kwanza alikua hana idea hata kama yanarekodiwa, sasa Boss na
kiongozi wa Janja ambaye ni Madee ameyasikia yale matusi na anatueleza mkasa mzima na kinachofuata kwenye video hii hapa chini.
Unaweza kuisikiliza sauti yenyewe ya maongezi ya simu ya Dogo Janja na Msichana aliyekuwa akimtongoza

Note: Only a member of this blog may post a comment.