Monday, December 7, 2015

Anonymous

Babu Aoa na Kumbaka Mtoto wa Miaka 8 Huko Bunda...Kilichomkuta ni Hiki....

Mahakama ya Bunda amemhukumu kifungo cha miaka 30 jela Changwe Changige mwenye miaka 54 kwa kosa la kumuoa na kumbaka mtoto wa miaka minane.
Wakati huo huo mahakama hiyo imemhukumu baba wa mtoto huyo kifungo cha miaka mitatu kwa kosa la kuruhusu mtoto huyo kuolewa.

Watuhumiwa hao walitenda kosa hilo Junuari mwaka jana katika kijiji cha Nyaburundu.
Akitoa hukumu hiyo hakimu wa mahakama hiyo alisema watuhumiwa hao watakwenda jela pamoja na adhabu hizo zitakwenda pamoja.

Mwendesha mashtaka alieleza kuwa washtakiwa hao walikula njama na kumuoza mtoto huyo kwa siri huku muhusika akitumia nafasi ya kumuoa mtoto huyo kwa kumbaka na kumsababishia maumivu makali.

USIPITWE! JIUNGE NASI FACEBOOK

Subscribe to this Blog via Email :

TOA MAONI YAKO HAPA (MATUSI HAYARUHUSIWI)

Note: Only a member of this blog may post a comment.