Saturday, October 24, 2015

Anonymous

VIDEO&PICHAZ: Matokeo ya Mechi Zote za Ligi Kuu Uingereza Leo October 24

Ligi Kuu Uingereza imeendelea kwa michezo kadhaa kupigwa katika viwanja tofauti tofauti, miongoni mwa michezo iliyokuwa inapewa nafasi kubwa au kuteka hisia za mashabiki wengi wa soka ni mechi kati ya Arsenal dhidi ya Everton, mchezo ambao umepigwa katika dimba la Emirates.
during the Barclays Premier League match between Arsenal and Everton at Emirates Stadium on October 24, 2015 in London, England.
Arsenal ambao wanafundishwa na kocha wa Kifaransa aliyedumu na klabu hiyo kwa zaidi ya miaka 10 wamefanikiwa kupata ushindi katika uwanja wao wa nyumbani, ushindi ambao umewafanya Arsenal kutimiza jumla ya point 22 na kushika nafasi ya kwanza katika msimamo wa Ligi.
during the Barclays Premier League match between Arsenal and Everton at Emirates Stadium on October 24, 2015 in London, England.
Timu ya Arsenal imefanikiwa kushinda kwa jumla ya goli 2-1, magoli ambayo yalifungwa na Olivier Giroud kwa kichwa dakika ya 36 kabla ya dakika mbili mbele beki wa klabu hiyo Laurent Koscielny kupachika goli la pili, kwa upande wa Everton walipata goli la kufutia machozi kupitia kwa Ross Barkley dakika ya 44 ya mchezo.
mimi
Matokeo ya mechi za Ligi Kuu Uingereza zilizochezwa October 24
Video ya magoli ya mechi ya Arsenal Vs Everton
Video ya magoli ya West Ham United Vs Chelsea

USIPITWE! JIUNGE NASI FACEBOOK

Subscribe to this Blog via Email :

TOA MAONI YAKO HAPA (MATUSI HAYARUHUSIWI)

Note: Only a member of this blog may post a comment.