Thursday, October 29, 2015

Anonymous

TAARIFA za Mbunge IRENE UWOYA Kufariki Zasababisha Usumbufu Mkubwa Kwenye Familia Yake!

Taarifa za uzushi zilizoandikwa jana kwenye Facebook kuwa muigizaji wa filamu, Irene Uwoya amefariki, zinadaiwa kusababisha usumbufu mkubwa kwenye familia yake.

Uzushi huo umekanushwa na kulaaniwa vikali na muigizaji mwenzake, Jacob Stephen aka JB.
“Ndugu zangu jana kupitia akaunti feki ya facebook kuna mtu alitoa picha yangu nikilia na kusema Irene Uwoya amefariki,” ameandika JB kwenye Instagram.
“Habari hii ya uongo ilileta shida kubwa katika familia yake na watu wa karibu. Leo tena asubuhi mwingine kasema nimepata ajali nakusababisha tafrani kubwa,” aliongeza.
“Napenda kuwaambia mashabiki wetu kuwa habari hizo ni za uongo. Tuko fiti kwa damu ya Yesu na tunavunja roho hizo za kunenea watu mabaya ktk jina la Yesu..amen.”

USIPITWE! JIUNGE NASI FACEBOOK

Subscribe to this Blog via Email :

TOA MAONI YAKO HAPA (MATUSI HAYARUHUSIWI)

Note: Only a member of this blog may post a comment.