Monday, August 17, 2015

Anonymous

NG'OMBE HAZEEKI MAINI! Khadija Kopa Sasa Yupo Tayari Kuolewa Tena! Amefunguka VIGEZO Hapa...

DSC_1452

Malkia wa Mipasho Afrika Mashariki na Kati, Khadija Omary Kopa ‘Da’ Khadija’.
Kutoka moyoni! Malkia wa Mipasho Afrika Mashariki na Kati, Khadija Omary Kopa ‘Da’ Khadija’ amefunguka la moyoni kwamba sasa yupo tayari kuolewa tena iwapo atatokea mwanaume mwenye vigezo anavyovihitaji. 

Kwa mujibu wa Khadija, pamoja na kwamba yupo tayari kuolewa lakini hahitaji mwanaume suruali bali mchapakazi, mwenye upendo wa kweli kama alivyokuwa aliyekuwa mumewe, marehemu Jafarry Ally.
“Kuolewa ni jambo la kheri, hakuna asiyelipenda lakini mimi sipendi mwanaume asiyependa maendeleo anayependa kuoa ilimradi kaoa, napenda atakayeshirikiana na mimi kwenye kila kitu,” alisema Khadija.

USIPITWE! JIUNGE NASI FACEBOOK

Subscribe to this Blog via Email :

TOA MAONI YAKO HAPA (MATUSI HAYARUHUSIWI)

Note: Only a member of this blog may post a comment.