Wednesday, October 14, 2015

Anonymous

ROSE NDAUKA: Sijihusishi na Kampeni UCHAGUZI MKUU Kwa Sababu Sitaki Kuwachanganya Mashabiki!

Ndauka.jpg 
Gladness Mallya
MWANADADA staa wa filamu Bongo, Rose Ndauka amesema hataki kujihusisha na harakati za siasa kwa sasa kwa vile anaogopa kuwachanganya mashabiki wake. 
Akipiga stori na gazeti hili, Rose alisema kwa kuwa yeye ni kioo cha jamii anayeelimisha kupitia kazi yake, alisema kujiweka wazi upande ulipo ni kuwagawa watu wake kitu ambacho asingependa kitokee.
“Wasanii wanaozunguka kwenye kampeni hawafanyi vibaya, lakini mimi siwezi na sikutaka kufanya hivyo ila kura nitapiga na kuhusu ni nani nitakayemchagua kuwa rais ni siri yangu,” alisema nyota huyo ambaye anakiri kuwa soko lao limeyumba.

USIPITWE! JIUNGE NASI FACEBOOK

Subscribe to this Blog via Email :

TOA MAONI YAKO HAPA (MATUSI HAYARUHUSIWI)

Note: Only a member of this blog may post a comment.