Saturday, October 24, 2015

Anonymous

Je, Kama Mtu Aliyejiandikisha Arusha na Yuko Kikazi Dar Nini Kifanyike Kupiga Kura? Majibu Yako Hapa….

Najua kuna watu mtakuwa mnataka kufahamu kwamba, Je kama mtu aliyejiandikisha Dar es Salaam  na yupo Arusha kikazi atafanye? ,majibu yako hapa yamejibiwa na Mkurugenzi wa huduma za kisheria wa tume ya Uchaguzi, Emmanuel Kawishe. 

‘Mtu atapigia kura mahali ulipojiandikisha kama ulijiandikisha Dar es Salaam hakikisha unarudi kuja kupigia kura Dar es Salaam  kwa hiyo hatoruhusiwa mtu kwa mujibu wa sheria kupigia kura sehemu yoyote kifungu  cha 91 kifungu kidogo cha tatu A kinasema mtu ataenda sehemu ya kujiandisha na kuruhusiwa kupiga kura’ – Emmanuel Kawishe 

‘Kwa hiyo kama mtu akiwa Dar es Salaam labda amejiandikisha Arusha anachotakiwa ni kufanya maamuzi ya kwenda Arusha kwenda kituo alichojiandikisha ndipo aweze kushiriki kupiga kura’ – Emmanuel Kawishe
Unaweza ukabonyeza play kumsikiliza Mkurugenzi wa huduma za kisheria wa tume ya Uchaguzi, Emmanuel Kawishe.

USIPITWE! JIUNGE NASI FACEBOOK

Subscribe to this Blog via Email :

TOA MAONI YAKO HAPA (MATUSI HAYARUHUSIWI)

Note: Only a member of this blog may post a comment.