Sunday, October 18, 2015

Anonymous

HATARI! Mgombea wa CHADEMA Awekewa Bomu Kwenye Gari Lake!


Mbunge wa Musoma mjini, CHADEMA, anayetetea kiti hicho, leo amekuta bomu la Kutengeneza katika moja ya gari anazotumia katika Kampeni zake.
Akithibitisha habari hizo amesema, ''bomu la kutengenezwa lilitegwa kwenye gari langu leo kwa ajili ya kuondoa maisha yangu, Mungu amekataa hila chafu''  
Bomu hilo lilitegwa katika gari analotumia yeye kwenye kampeni zake. Vincent Nyerere mbali na kwamba ni mgombea ubunge wa Musoma mjini, ndiye mwenyekiti wa CHADEMA mkoa wa Mara, na ni miongoni mwa wanasiasa wenye nguvu na ushawishi mkubwa sana katika siasa za upinzani mikoa ya kanda ya ziwa.

USIPITWE! JIUNGE NASI FACEBOOK

Subscribe to this Blog via Email :

TOA MAONI YAKO HAPA (MATUSI HAYARUHUSIWI)

Note: Only a member of this blog may post a comment.