
MWENYEKITI Mtendaji wa Makampuni ya IPP, Dk Reginald Mengi amesema kuwa taarifa zinazosambazwa kwenye mitandao ya kijamii kuwa yeye amejitoa kwa Lowasa si za kweli.
Alisema hayo kwa waandishi wa habari, aliokutana nao jijini Dar es Salaam, jana.
Alikutana na waandishi hao ili kufafanua kuhusu taarifa, aliyosema inaenezwa kupitia mitandao ya kijamii, yenye kichwa cha habari ‘Mengi ajitoa rasmi kwa Lowassa’. Edward Lowassa ni mgombea urais wa Chadema anayeungwa mkono na vyama vinavyounda Ukawa.
Mbali na Chadema, vyama vingine katika Ukawa ni CUF, NCCR-Mageuzi na NLD.
Taarifa yake aliyosoma kwa waandishi wa habari kuhusu suala hilo ilisema:
Dk Mengi alisema “Taarifa hiyo ni ya uongo, upotoshaji na uchochezi”. Dk Mengi alieleza kuwa “Taarifa za aina hii zisipokemewa na kuchukuliwa hatua za haraka, zitaathiri amani ya Taifa letu. Ni matarajio yangu kwamba vyombo husika vitachukua hatua zinazostahili kwa haraka iwezekanavyo”.

Note: Only a member of this blog may post a comment.