Wednesday, October 14, 2015

Anonymous

Baada ya Kutumia Mamilioni Katika Usajili, Huu ni Msimamo wa MANCHESTER United Katika Kujenga Timu Yao!


Klabu ya Manchester United ya Uingereza ni moja kati ya vilabu vilivyotumia fedha nyingi katika dirisha la usajili lililofungwa mwezi August 2015. Toka kocha Louis van Gaal ajiunge na klabu ya Man United, uongozi wa klabu hiyo umetumia zaidi ya pound milioni 250 kwa ajili ya kusajili wachezaji.

Ed Woodward
Man United inaonekana kufanya usajili kwa malengo ya baadae zaidi kwani imekuwa ikisajili wachezaji wenye umri mdogo kama Memphis Depay, Anthony Martial na Morgan Schneiderlin. Stori kutoka kwa makamu mwenyekiti wa klabu hiyo Ed Woodward kuhusu matumizi hayo ya fedha yaliyotumika katika usajili.

Ed Woodward amekiri kuwa bado Manchester United itaendelea na matumizi ya fedha nyingi kwa ajili ya kuimarisha kikosi chake, Ed Woodward amesema Man United katika dirisha la usajili lililofungwa mwezi August walikuwa wakihusishwa kutaka kusajili wachezaji wengi zaidi lakini walifanikiwa kusajili sita. Hivyo Man United bado itaendelea kutumia fedha nyingi katika usajili ili kuimarisha kikosi.

USIPITWE! JIUNGE NASI FACEBOOK

Subscribe to this Blog via Email :

TOA MAONI YAKO HAPA (MATUSI HAYARUHUSIWI)

Note: Only a member of this blog may post a comment.