WATU 40 wakiwemo
watalii na dereva mmoja wa lori wamefariki dunia na watano kujeruhiwa na
wengine wanane kunusurika baada ya basi lao kugongana na lori na yote
kuwaka moto palepale katika barabara moja Kusini Magharibi mwa Ufaransa.
Ajali hiyo imetokea karibu na Puisseguin
eneo la Gironde Mashariki mwa Bordeaux, muda mfupi baada ya basi hilo
kuanza safari kutoka mji wa jirani. Wengi wa waliokuwa kwenye basi hilo
walitoka chama cha wazee kilicho katika mji wa
Petit-Palais-et-Cornemps.
Rais wa Ufaransa Francois Hollande
ameandika kwenye Twitter kwamba serikali “imechukua hatua zote
kushughulikia mkasa huo mbaya”.
Mkasa huo ndio mbaya zaidi kutokea barabarani nchini humo tangu ajali iliyoua watu 52 iliyotokea mwaka 1982.
Mpaka sasa chanzo cha ajali hiyo bado
hakijabainika wakati Waziri Mkuu wa Ufaransa Manuel Valls, pamoja na
mawaziri wa masuala ya ndani na uchukuzi wanatarajiwa kutembelea eneo la
mkasa.

Note: Only a member of this blog may post a comment.