Dustan Shekidele, Morogoro
MSALA! Warembo kadhaa wenyeji wa mji wa Morogoro Ijumaa
iliyopita walishiriki kufanya shindano la aibu linalodaiwa kuandaliwa na
viongozi wa serikali ya mtaa na kufanyika katika Ukumbi wa Shirati,
wakicheza na kutembea nusu utupu jukwaani.
Shindano
hilo maarufu kama Kanga Moko lilisababisha wananchi kukerwa na hivyo
kuwaita askari, ambao hata hivyo, walishindwa kulizuia tukio hilo
lililofanyika katika Mtaa wa Tupendane, Chamwino na mgeni rasmi akiwa ni
kigogo wa mtaa aliyetajwa kwa jina moja la Milomo.
Gazeti
hili lilishuhudia viongozi hao wa serikali wakifurahia mabinti hao
wakishindana kufanya shoo hiyo ya nusu utupu. Baada ya hapo washiriki
hao walipita jukwaani wakiwa na khanga moja waliyojifunga upande mmoja
huku upande wa pili wakiwa watupu,” kabla ya askari wawili kutinga
ukumbini hapo, lakini viongozi wa serikali ya mtaa wakazungumza nao
‘kiutu uzima’ na kuliacha zoezi hilo likiendelea.
Katika
shindano hilo, Grace John aliyekuwa kinara wa kukaa kihasarahasara
alishinda na kuwa Miss Shirati Khanga Part 2015 akimrithi Merry Oddo
aliyetwaa taji hilo mwaka jana, Latifa Selemani alitwaa nafasi ya pili
na Zamida Hemedi alishika nafasi ya tatu ambapo mgeni rasmi wa shindano
hilo, Papaa Milomo alikabidhi zawadi kwa washindi hao.
Note: Only a member of this blog may post a comment.