Thursday, September 24, 2015

Anonymous

Rais MWAKIFWAMBA Awatemea Cheche Wasanii TZ

mwakifwamba
Gladness Mallya
RAIS wa Shirikisho la Filamu Tanzania ‘TAFF’, Simon Mwakifwamba amewatemea cheche wasanii na kuwataka kuachana na kuendekeza kupokea fedha za wanasiasa tu bila kutetea masilahi yao.
Akistorisha na paparazi wetu, Mwakifwamba alisema kwa sasa tasnia ya filamu imekufa kabisa hivyo wasanii wanaopata nafasi ya kuzunguka na wagombea urais wawe wanawaambia na matatizo waliyonayo kuliko kuishia kuchekelea fedha wanazopewa na kusahau kazi yao ilivyo na changamoto nyingi. 
“Kama wanalipwa ni jambo zuri sana lakini pia watumie fursa hiyo kutetea masilahi ya tasnia wasijisahau kutokana na fedha wanazopata kwani uchaguzi utaisha na maisha yataendelea,” alisema Mwakifwamba.

USIPITWE! JIUNGE NASI FACEBOOK

Subscribe to this Blog via Email :

TOA MAONI YAKO HAPA (MATUSI HAYARUHUSIWI)

Note: Only a member of this blog may post a comment.