Gladness Mallya
RAIS wa Shirikisho la Filamu Tanzania ‘TAFF’, Simon Mwakifwamba amewatemea cheche wasanii na kuwataka kuachana na kuendekeza kupokea fedha za wanasiasa tu bila kutetea masilahi yao.
Akistorisha na paparazi wetu, Mwakifwamba alisema kwa sasa tasnia ya
filamu imekufa kabisa hivyo wasanii wanaopata nafasi ya kuzunguka na
wagombea urais wawe wanawaambia na matatizo waliyonayo kuliko kuishia
kuchekelea fedha wanazopewa na kusahau kazi yao ilivyo na changamoto
nyingi.
“Kama wanalipwa ni jambo zuri sana lakini pia watumie fursa hiyo kutetea masilahi ya tasnia wasijisahau kutokana na fedha wanazopata kwani uchaguzi utaisha na maisha yataendelea,” alisema Mwakifwamba.
RAIS wa Shirikisho la Filamu Tanzania ‘TAFF’, Simon Mwakifwamba amewatemea cheche wasanii na kuwataka kuachana na kuendekeza kupokea fedha za wanasiasa tu bila kutetea masilahi yao.
“Kama wanalipwa ni jambo zuri sana lakini pia watumie fursa hiyo kutetea masilahi ya tasnia wasijisahau kutokana na fedha wanazopata kwani uchaguzi utaisha na maisha yataendelea,” alisema Mwakifwamba.

Note: Only a member of this blog may post a comment.