Jengo la kisasa la mfuko wa pensheni kwa watumishi wa umama-PSPF.
Rais Jakaya Kikwete amezindua jengo la
kisasa la mfuko wa pensheni kwa watumishi wa umama-PSPF- na kuyataka
mashirika mengine nchni kujenga majengo ya kisasa ili kuleta imani na
matumaini kwa wawekezaji kuwa Tanzania ina mazingira mazuri ya
uwekezaji.
Akizungumza katika uzinduzi huo, rais Kikwete licha ya kupongeza
bodi ya wadhamini kwa kubuni wazo la kujenga jengo hilo,amesema jengo
hilo limebadili mandhari ya jiji la Dar es Salaam na ni alama inayoweza
kuvutia na kujenga matumaini kwa wawekezaji wanakuja nchini.
Rais Jakaya Kikwete akizindua jengo la kisasa la mfuko wa pensheni kwa watumishi wa umama-PSPF
Naibu waziri wa fedha Mhe. Adam Malima amesema ujenzi wa jengo hilo
ni utekelezaji wa sera ya uwekezaji ambapo ameitaka PSPF kulitumia kama
kitegeuchumi ambapo kutia halfa hiyo ameahidi serikali italipa madeni
yote yanayodaiwa na mashirika ya hifadhi katika kipindi kifupi kijacho.
Mwenyekiti wa bodi ya wadhamani wa mfuko wa pensheni kwa watumishi
wa umama-PSPF-Bwana George Yembesi amepongeza serikali ya awamu ya nne
kwa kuhamaisha uwekezaji uliohamasisha mfuko wa PSPF kubuni na
kukamilisha jengo ambapo amesema moja ya changamoto kubwa inayoukabiri
mfuko wa PSPF ni deni kubwa linaloidai serikali na kuitaka lilipwe kabla
ya kukamilika kwa uongozi wa serikali ya awamu ya nne.
Majengo pacha ya mfuko wa pensheni kwa watumishi wa
umama-PSPF-lina urefu wa mita 147 ni jengo refu la kwanza katika nchi
wanachama wa jumuiya ya Afrika mashariki na ni jengo la nane kwa urefu
katika bara la Afrika mpaka kukamilika limegharimu zaidi ya shilingi
bilioni 139.2.

Note: Only a member of this blog may post a comment.