Thursday, September 10, 2015

Anonymous

Mastaa na Uchaguzi 2015

Shani Ramadhani
Kulwa Kikumba ‘Dude’
Kampeni zinaendelea vizuri katika kila upande na hata yale maneno yanayoongelewa ni utani kama ule uliop kwenye timu za mpira wa Yanga na Simba, changamoto kubwa iliyopo ni kwa wapiga kura kwa sababu wanatakiwa kuangalia sera muhimu kama afya na elimu kutoka kwa wagombea wao.
Fatuma Ayubu ‘Bozi’
Kwangu naona muelekeo wa kampeni ni mzuri lakini tunaomba hali ya amani na utulivu iwe hivi hivi mpaka siku ya uchaguzi itakapofika ili tupate kuchagua viongozi sahihi watakaotuwakilishia matatizo yetu huko bungeni.
Haji Adam ‘Baba Haji’
Muonekano wa kampeni kuelekea uchaguzi mkuu uko vizuri sana tu sema wanatuharibia wale watu wanaotumia muda huu kutoa kauli chafu zenye kuwakera watu badala ya kutangaza sera muhimu kwa wananchi kwa sababu wao ndiyo waamuzi.
Mohammed Mwikongi ‘Frank’
Kampeni za mwaka huu ni tofauti na za miaka iliyopita kwa sababu  kuna muamko mkubwa kutoka kwa akina mama na vijana ambao wengi wao wana kiu ya kupata mabadiliko na hata idadi ya wapiga kura nayo inaonekana kuwa kubwa.

USIPITWE! JIUNGE NASI FACEBOOK

Subscribe to this Blog via Email :

TOA MAONI YAKO HAPA (MATUSI HAYARUHUSIWI)

Note: Only a member of this blog may post a comment.