Friday, September 11, 2015

Anonymous

Kisa LOWASSA, MAGUFULI…KITALE, MAFUFU Wamwagiana MATUSI!

Kitale
Muigizaji maarufu Bongo, Musa Yusuf ‘Kitale au Mkude Simba’.
Gladness Mallya na Hamida Hassan
SIASA zitawatoa roho mastaa! Waigizaji maarufu Bongo, Musa Yusuf ‘Kitale au Mkude Simba’ na Jimmy Mafufu wamejikuta wakitukanana chanzo cha yote kikitajwa kuwa ni mambo ya siasa.
jimmyymafufucutMuigizaji maarufu Bongo, Jimmy Mafufu.
Mtoa habari aliyeomba hifadhi ya jina lake alilitonya Ijumaa kwamba, mwanzo wa uhasama wao ni baada ya Mafufu kumuunganisha Kitale na Ukawa kama mmoja wa wasanii wanaounga mkono umoja huo lakini baadaye Kitale akarudi kumuunga mkono mgombea kutoka CCM, Mhe. John Magufuli.
“Unajua Kitale alijua kuwa kule Ukawa msanii akienda anapewa mpunga, sasa alipoona mambo siyo mambo, akajirudia zake kwenye chama la nyumbani (CCM) ndipo bifu lilipoanzia. 

Baada ya kupata habari hizo, gazeti hili lilimtafuta Kitale na kumsomea madai hayo ambapo alikuwa na haya ya kusema:
“Achana na huyo Mafufu sitaki kumzungumzia naona anatafuta umaarufu, kila mtu ana uhuru wa kuwa chama anachokitaka, nimwambie tu siasa zitapita na maisha yataendelea kama kawaida, mwache aendelee kuongea.”
Kwa upande wa Mafufu alipotafutwa alisema: “Kitale ni mjinga alikuja kuniomba nimuunganishe na Lowassa, nikafanya hivyo baada ya kuja alidhani kuna hela akaamua kuondoka.”

USIPITWE! JIUNGE NASI FACEBOOK

Subscribe to this Blog via Email :

TOA MAONI YAKO HAPA (MATUSI HAYARUHUSIWI)

Note: Only a member of this blog may post a comment.