Thursday, September 17, 2015

Anonymous

KADINDA Amdhalilisha Vibaya KAJALA

Kadinda-3Mwanamitindo na Meneja wa mcheza filamu Wema Sepetu, Martin Kadinda.
Imelda Mtema
DHARAU! Meneja wa mcheza filamu Wema Sepetu, Martin Kadinda ambaye pia ni mwanamitindo, katika hali isiyo ya kawaida, amemdhalilisha rafiki kipenzi wa zamani wa bosi wake huyo, Kajala Masanja kwa kumwelezea kuwa historia za maisha yao ni tofauti mno, kitu kinachotoa picha kuwa urafiki wao usingeweza kudumu.
c367kajala8891Staa wa filamu za Bongo, Kajala Masanja ‘Kay’.
Akizungumza na gazeti hili hivi karibuni, Kadinda alisema makuzi ya mastaa hao wawili kuanzia shule na aina ya maisha ni vitu viwili tofauti na hawaendani, kwani hata urafiki wao haukutoka moyoni, bali ulisukumwa na upendo wa mtoto wa Kajala kwa Wema.
“Kajala kasoma uswahilini na Wema kama unavyojua, kapata elimu yake ya uhakika kwenye shule za maana, hata maisha yao ya kawaida unaona yana tofauti kubwa, kama siyo Paula (mtoto wa Kajala) kumpenda Wema, wawili hawa wasingeweza kuwa marafiki,” alisema Kadinda. 

Gazeti hili lilimtafuta Kajala ili kuzungumzia maneno hayo ambapo alionyesha kusikitishwa kwake na kauli hiyo, akidai kwa kipindi chote wao wakiwa marafiki, hakuwahi kuona Kadinda akitilia shaka urafiki wao.
“Daah mimi hata nashindwa nizungumzeje, simuelewi kabisa huyo meneja maana yeye huko nyuma sikuwahi kusikia akisema hivyo, amenishangaza sana na bado nitaendelea kumshangaa,” alisema Kajala. 

Kadinda alitoa kauli hiyo alipotakiwa kuzungumzia urafiki wa bosi wake na staa mwingine wa filamu, Yobnesh Yusuf ‘Batuli’ kwani historia inaonyesha Wema hadumu na marafiki.
“Ki ukweli kabisa urafiki wa Wema na Batuli mimi naukubali kwa asilimia zote kabisa, kwa kuwa Batuli anapenda kufanya mambo yake ‘private’ na maisha hayo ndiyo staa anapaswa kuyaishi, kuliko kuyaanika kila wakati maana watu lazima wakuchoke” alisema Kadinda.

USIPITWE! JIUNGE NASI FACEBOOK

Subscribe to this Blog via Email :

TOA MAONI YAKO HAPA (MATUSI HAYARUHUSIWI)

Note: Only a member of this blog may post a comment.