Thursday, September 24, 2015

Anonymous

JUX Adai Hawezi Kufanya Show za Kampeni za KISIASA

Mwimbaji wa muziki wa R&B, Jux amesema hawezi kufanya show za kampeni za kisiasa kwa kuogopa kuwachanganya mashabiki wake.

3b4c0a35c503b6623a260af30d902861
Akizungumza na kipindi cha Planet Bongo cha EATV, Jux alisema akipanda kwenye majukwaa ya siasa itakuwa ni kama anawashinikiza mashabiki wake kuchagua viongozi wasiowataka.
“Watanzania tulivyo, mimi kama kuna mtu ananipenda mpaka akaamua kuchora Jux au akaandika Jux kwenye mwili wake, mtu huyo nina nguvu ya kumshawishi na akafanya kitu bila ya yeye kutaka,” alisema.
“Kwahiyo leo nikisimama kwenye stage nikasema tumchague mtu fulani, kuna watu wengi sana katika akili zao watasema hata Jux mwenyewe kamchagua mtu fulani. Ndio maana hata viongozi wa siasa kwenye kampeni zao wanachagua wasanii ili kushawishi.

Kwahiyo mimi naomba kama shabiki wangu uniangalia, mimi mwenyewe ni siri yangu, kuna kiongozi ambaye namuamini. Lakini wewe angalia mwenyewe, nenda Chadema au CCM. Msikilize Magufuli au Lowassa, wewe si una akili?”

USIPITWE! JIUNGE NASI FACEBOOK

Subscribe to this Blog via Email :

TOA MAONI YAKO HAPA (MATUSI HAYARUHUSIWI)

Note: Only a member of this blog may post a comment.