Ben Pol na muimbaji mrembo wa Kenya, Avril huenda wakaingia ama tayari wameingia studio kurekodi ngoma ya pamoja.
Wawili hao wameshare picha kwenye akaunti zao za Instagram na kuelezea kile kinachowezekana kuwa ni ujio wa collabo yao.
“Throwback hanging out with the talented @iambenpol…we just might have a surprise for you. #255 #254,” ameandika Avril.
Naye Ben ameandika: #throwback with @theavieway #avril ..unaonaje
mimi na Avril tukiingia Studio na kuimba wimbo pamoja?, hmm I guess
itakuwa wimbo mtamu sana kissing_smiling_eyes, we unaonaje? Maoni mengi
yakiwa positive Nitamuomba Avril tufanye.”
Sio mara ya kwanza kwa Avril kufanya collabo na wasanii wa Tanzania. Amewahi kufanya wimbo na AY na Ommy Dimpoz.

Note: Only a member of this blog may post a comment.