Wednesday, August 12, 2015

Anonymous

USAJILI ULAYA: Hatimaye Pedro Rodriguez amechukua uamuzi huu kuhusu uhamisho wake.

Namba ya siku Pedro atakazoendelea kukaa ndani ya klabu ya FC Barcelona zinahesabika baada ya Rafinha kupewa nafasi ya kuanza katika kikosi cha kwanza kinachocheza na Sevilla katika Spanish Supercup. 
Pedro mwenye asili ya visiwa vya Canary, amekuwa akihusishwa na kujiunga na Manchester United, na usiku wa leo kocha Luis Enrique alimuweka benchi huku mkurugenzi wa michezo wa timu hiyo Robert Fernandez amekiambia kituo cha Esport 3 kwamba Pedro ameomba kuhama.
“Pedro amenitaarifu rasmi kwamba anataka kuondoka, ila kwa sasa bado hatujapata ofa. Ikiwa kuna klabu inayomtaka basi itabidi walipe fedha ya kuweza kuvunja mkataba wake ambayo ni £21m.”
  Klabu ya Manchester United inaripotiwa kuwa kwenye mazungumzo ya kina na Barcelona na muda wowote kutoka sasa inatarajiwa wataafikiana juu ya uhamisho huo.

USIPITWE! JIUNGE NASI FACEBOOK

Subscribe to this Blog via Email :

TOA MAONI YAKO HAPA (MATUSI HAYARUHUSIWI)

Note: Only a member of this blog may post a comment.