Brighton Masalu
MCHEKESHAJI maarufu, Steven Mengere
‘Steve Nyerere’ amesema atakuwa mbunge ombaomba kwa wadau, serikali na
mashirika binafsi katika kutatua matatizo mbalimbali ya Jimbo la
Kinondoni.
Akizungumza na mwandishi wetu hivi
karibuni, msanii huyo alisema ana uzoefu wa kuomba, hivyo hataona haya
kutumia kipaji chake cha kushawishi katika kuomba mafanikio na anaamini
yeye ni jibu sahihi kwa wananchi wa Kinondoni.
“Mimi nina ushawishi mkubwa sana, hivyo
nitatumia kipaji hicho kuishawishi serikali, wadau na mashirika ya umma
kuomba misaada mingi, hakika nitakuwa mbunge ombaomba,” alisema Nyerere.

Note: Only a member of this blog may post a comment.