Jeshi la Polisi Mkoa wa Ilala linamshikilia mtu mmoja anayedaiwa kuhusika na shambulio lililofanywa na wafuasi wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), ambalo lililotokea Msongola kijiji cha Kidole, Chanika na kusababisha watu kujeruhiwa na wanawake kudhalilishwa.
Vurugu hizo zinadaiwa kufanywa na moja ya kundi la watia nia Jimbo la Ukonga.
Kwa mujibu wa Kamanda wa Mkoa wa Ilala, Lucas Mkondya alisema, tukio hilo lilitokea juzi alasiri wakati wafuasi wa kundi la mtia nia mmoja lilipovamia na kuliteka gari lililokuwa limebeba wafuasi wa CCM.
Alisema walioshambuliwa walikuwa kwenye gari aina ya Noah ambao walikuwa wanatoka kwenye mkutano na walipofika eneo hilo walikutana na gari aina ya Jeep ambalo watu waliokuwamo ndani walifanya unyama huo.
Kamanda alisema baada ya shumbulio, watu wanane waliokuwa kwenye Noah walitoa ripoti polisi zilizowezesha kukamatwa kwa mtu mmoja ambaye jina lake wamelihifadhi.
“Tunaendelea kumhoji mtu huyu kwa kesi iliyofunguliwa ya shambulio, kati ya waliofungua kesi wanawake ni wanne,” alisema.
Alisema jeshi la polisi linaendelea kufuatilia wengine waliohusika kwenye vurugu hizo.
Chanzo cha habari cha kuaminika kilichofanikiwa kufika eneo la tukio na kushuhudia waliofanyiwa unyama huo, baada ya watu hao kuliteka gari hilo walilipeleka kwenye vichaka na kuanza kuwavua nguo wanawake na kuwafanyia udhalilishaji huo.
Chanzo hicho kimesema kuwa, watu hao waliwajeruhi wanaume sita ambao mmoja alitobolewa tumboni na kukimbizwa hospitali ya Temeke kwa matibabu.
Chanzo kilieleza kuwa, waliotekwa walisema watekaji hao walikuwa wanawahoji kwa nini wameamua kumsapoti mgombea wa jimbo la Ukonga (jina tunalo).
Vurugu hizo zinadaiwa kufanywa na moja ya kundi la watia nia Jimbo la Ukonga.
Kwa mujibu wa Kamanda wa Mkoa wa Ilala, Lucas Mkondya alisema, tukio hilo lilitokea juzi alasiri wakati wafuasi wa kundi la mtia nia mmoja lilipovamia na kuliteka gari lililokuwa limebeba wafuasi wa CCM.
Alisema walioshambuliwa walikuwa kwenye gari aina ya Noah ambao walikuwa wanatoka kwenye mkutano na walipofika eneo hilo walikutana na gari aina ya Jeep ambalo watu waliokuwamo ndani walifanya unyama huo.
Kamanda alisema baada ya shumbulio, watu wanane waliokuwa kwenye Noah walitoa ripoti polisi zilizowezesha kukamatwa kwa mtu mmoja ambaye jina lake wamelihifadhi.
“Tunaendelea kumhoji mtu huyu kwa kesi iliyofunguliwa ya shambulio, kati ya waliofungua kesi wanawake ni wanne,” alisema.
Alisema jeshi la polisi linaendelea kufuatilia wengine waliohusika kwenye vurugu hizo.
Chanzo cha habari cha kuaminika kilichofanikiwa kufika eneo la tukio na kushuhudia waliofanyiwa unyama huo, baada ya watu hao kuliteka gari hilo walilipeleka kwenye vichaka na kuanza kuwavua nguo wanawake na kuwafanyia udhalilishaji huo.
Chanzo hicho kimesema kuwa, watu hao waliwajeruhi wanaume sita ambao mmoja alitobolewa tumboni na kukimbizwa hospitali ya Temeke kwa matibabu.
Chanzo kilieleza kuwa, waliotekwa walisema watekaji hao walikuwa wanawahoji kwa nini wameamua kumsapoti mgombea wa jimbo la Ukonga (jina tunalo).


Note: Only a member of this blog may post a comment.