Kazi yangu ni kukusogezea stori zote
kubwa zinazoweka headlines kwenye magazeti, hizi hapa ni baadhi ya
zilizoguswa kwenye Uchambuzi wa Redioni #OnAIR August 14 2015.
Polisi wazuia msafara wa Edward Lowassa kwenda Usangi Kilimanjaro kwenye msiba wa kada wa CCM, Peter Kisumo.. Jeshi la Polisi lapiga marufuku misafara kwenda kuchua fomu Ofisi za NEC pamoja na kwenye kusaka wadhamini…Prof.Lipumba arejea nchini kutoka Rwanda na ameapa kutokuunga mkono umoja wa UKAWA.
Mchujo wa CCM baadhi ya Wabunge wasalimika… Watuhumiwa wa Ujambazi Stakishari wakamatwa, Waziri wa Mambo ya Nje na ushirikiano wa Kimataifa, Benard Membe afunguka kuhusu kuanguka Urais CCM.
Maandamano ya CHADEMA yazuiwa Mbeya… Serikali imesema hakuna uthibitisho wowote wa ugonjwa wa EBOLA kuwepo Mkoani Kigoma, watu wa Kigoma watakiwa kuchukua tahadhari za muhimu dhidi ya ugonjwa huo.
Stori hizo na nyingine kubwakubwa ziko pia kwenye hii sauti niliyorekodi #PowerBreakfast @CloudsFM

Note: Only a member of this blog may post a comment.