Saturday, August 1, 2015

Anonymous

PICHAZ: Aunty, Iyobo mahaba niue zenji!

IMG-20150727-WA0016
Aunt Ezekiel Grayson Gwantwa na mzazi mwenzake, Moses Iyobo ‘Mo’ wakijiachia.
Imelda Mtema, aliyekuwa Zanzibar
MAHABA nifilisi. Aunt Ezekiel Grayson Gwantwa na mzazi mwenzake, Moses Iyobo ‘Mo’ wameonesha wazi kinachoitwa mapenzi ni kikohozi baada ya kujiachia kimahaba hadharani wakiwa sanjari na ‘mtoto wao’, Cookie jambo lililozua miguno mingi ya chinichini.
IMG-20150727-WA0022
Moses Iyobo ‘Mo’ akimbeba mtoto wao Cookie
Wawili hao walinaswa hivi karibuni visiwani Zanzibar, ambako kulikuwa na tamasha maalum la filamu (ZIFF), ambapo Aunt alikuwa miongoni mwa waalikwa huku Iyobo ‘akivamia shamba la bibi’ kwa kile alichodai ni kumpa kampani mwandani wake.
IMG-20150727-WA0023
“Unajua hii ndiyo safari yangu ya kwanza tangu nijifungue, kwa hiyo ni muda muafaka, ngoja tufurahie maisha kidogo jamani,” alisema Aunt.
IMG-20150727-WA0021

USIPITWE! JIUNGE NASI FACEBOOK

Subscribe to this Blog via Email :

TOA MAONI YAKO HAPA (MATUSI HAYARUHUSIWI)

Note: Only a member of this blog may post a comment.