Wednesday, August 12, 2015

Anonymous

Mwanasheria nguli ajitolea kumtetea SHILOLE dhidi ya adhabu ya BASATA

Huenda sasa Shilole anaweza kupata lepe la usingizi baada ya mwanasheria maarufu nchini, Albert Msando kuahidi kumsaidia kufuatia kupewa adhabu kali na baraza la sanaa la taifa, BASATA hivi karibuni.
11355156_470748403097550_1177631702_n
BASATA lilimfungia muimbaji huyo wa ‘Nakomaa na Jiji’ kutojihusisha na sanaa kwa mwaka mzima kutokana na kitendo chake cha kuidhalilisha nchi alipokuwa akitumbuiza nchini Ubelgiji.
Shishi amepost selfie Instagram akiwa na Msando na kuandika, “Nakuheshimu my kaka umeweza kujitoa kwa ajir yangu kwenye matatizo yangu! Mungu atakulipa inshaaalah @albertomsando.”
11856794_417122211811229_420751726_n Shilole na Msando
Bongo5 imempigia simu Shilole kutaka kupata maelezo ya ni kwa vipi mwanasheria huyo anamsaidia lakini amedai kuwa yeye si mzungumzaji wa jambo hilo.
Msando ni mwanasheria wa watu wengi mashuhuri akiwemo Zitto Kabwe.

USIPITWE! JIUNGE NASI FACEBOOK

Subscribe to this Blog via Email :

TOA MAONI YAKO HAPA (MATUSI HAYARUHUSIWI)

Note: Only a member of this blog may post a comment.