Gary Neville akiwa na marehemu baba yake.
BABA mzazi wa mastaa wawili wa soka, Gary na Phil Neville amefariki
dunia leo asubuhi baada ya kupatwa na shambulio la moyo akiwa safarini
kuelekea Australia.
Neville Neville.
Neville Neville, amefariki dunia akiwa na umri wa miaka 65.
Watoto wa marehemu, Gary na Phil ambao ni wachezaji wa zamani wa
Manchester United walikuwa pamoja na mzee wao leo asubuhi huko
hospitalini nchini Sydney kabla mauti kumfika.
Gary na Phil Neville.
Imeelezwa kuwa alifanyiwa upasuaji usiku wa kuamkia leo kujaribu kuokoa maisha yake.
Taarifa iliyotolewa na familia ya marehemu imesema hivi: “Tunapenda
kutoa shukrani kwa kila mmoja katika Hospitali ya St Vincent, Sydney kwa
kupigania uhai wa mzee wetu”.

Note: Only a member of this blog may post a comment.