Friday, August 7, 2015

Anonymous

MSIBA MANCHESTER UNITED: Baba mzazi wa wanasoka Gary na Phil Neville afariki!

neville-neville-pa
Gary Neville akiwa na marehemu baba yake.
BABA mzazi wa mastaa wawili wa soka, Gary na Phil Neville amefariki dunia leo asubuhi baada ya kupatwa na shambulio la moyo akiwa safarini kuelekea Australia.
Neville-Neville_2520352b
Neville Neville.
Neville Neville, amefariki dunia akiwa na umri wa miaka 65.
Watoto wa marehemu, Gary na Phil ambao ni wachezaji wa zamani wa Manchester United walikuwa pamoja na mzee wao leo asubuhi huko hospitalini nchini Sydney kabla mauti kumfika.
NEVILLE
Gary na Phil Neville.
Imeelezwa kuwa alifanyiwa upasuaji usiku wa kuamkia leo kujaribu kuokoa maisha yake.
Taarifa iliyotolewa na familia ya marehemu imesema hivi: “Tunapenda kutoa shukrani kwa kila mmoja katika Hospitali ya St Vincent, Sydney kwa kupigania uhai wa mzee wetu”.

USIPITWE! JIUNGE NASI FACEBOOK

Subscribe to this Blog via Email :

TOA MAONI YAKO HAPA (MATUSI HAYARUHUSIWI)

Note: Only a member of this blog may post a comment.