Monday, August 24, 2015

Anonymous

MH. DAVID KAFULILA NA MGOMBEA UBUNGE KUPITIA CCM KIMENUKA HUKO KIGOMA!

MGOMBEA Ubunge kwa tiketi ya Chama cha Mapinduzi, CCM, Jimbo la Kigoma Kusini, Hasna Sudi Mwilima, amewekewa pingamizi na mbunge anayemaliza muda wake katika jimbo hilo kwa tiketi ya Chama cha NCCR-Mageuzi, David Kafulila.

Mgombea huyo amewekewa pingamizi hilo kwa kushindwa kujaza fomu kwa kufanya makosa matatu ya kisheria. Kwa mujibu wa chanzo chetu cha habari:
  1. Kosa namba moja kwenye fomu 8B ametumia majina matatu tofauti: HASNA SUDI KATUNDA MWILIMA, HASNA MWILIMA na HASNA S. K. MWILIMA. 
  2. Aidha kosa namba mbili kwenye tamko la wadhamini imeandikwa amedhaminiwa kuteuliwa tarehe 25.10.2015 badala ya tarehe 21.8.2015.
Sheria inamtaka mgombea ajaze majina yake kamili na kwa mazingira hayo mgombea huyo hajulikani majina yake kamili ni yapi, vinginevyo anatakiwa kupeleka document iitwayo “deed poll” inayotambua majina yote hayo kuwa ni yake.

Kufuatia mkanganyiko huo David Kafulila jana jioni aliweka pingamizi dhidi ya mgombea huyo na kudai kuwa anapswa kuenguliwa kwenye uchaguzi mkuu ujao.

USIPITWE! JIUNGE NASI FACEBOOK

Subscribe to this Blog via Email :

TOA MAONI YAKO HAPA (MATUSI HAYARUHUSIWI)

Note: Only a member of this blog may post a comment.