Thursday, August 20, 2015

Anonymous

KUFURU! Nicki MINAJ na Mpenzi Wake, Meek Mill Wakodi Ukumbi Mzima Kutazama Muvi Wao Wawili Tu!

Marapa Nicki Minaj na Meek Mill ambaye ni mpenzi.
New York, Marekani
WAKATI, marapa Nicki Minaj na Meek Mill ambaye ni mpenzi wake wakitegemewa kumaliza ziara yao ya The Pinkprint waliyoianza tangu mwezi uliopita,wameendelea kufanya vituko baada ya hivi karibuni kokodi ukumbi kwa ajili ya kutazama muvi inayoitwa Staight Outta Compton,wakiwa wawili tu.
Tukio hilo linalojenga vichwa vya habari kwenye anga la burudani kwa sasa,lilitundikwa na Nick kwenye ukurasa wake wa Instagram baada ya kuposti picha wakiwa wawili tu, yeye na Meek Mill kwenye ukumbi ambao hakuutaja jina na kuambatanisha chini yake maandishi yaliyosomeka;“
Ni lini wewe na mpenzi wako mtakodi ukumbi mzima kuangalia muvi ya Staight Outta Compton?” alimaliza Nick Minaj kwa kumsifia pia mmoja wa waigizaji ambao wako ndani ya sinema hiyo akiwemo rapa Ice Cube

USIPITWE! JIUNGE NASI FACEBOOK

Subscribe to this Blog via Email :

TOA MAONI YAKO HAPA (MATUSI HAYARUHUSIWI)

Note: Only a member of this blog may post a comment.