Tuesday, August 18, 2015

Anonymous

Elewa Undani wa Ugonjwa wa Kifua Kikuu (TB)

TB (2)Kifua kikuu ambacho ni maarufu kwa kuitwa TB, ni ugonjwa unaosababishwa na kiumbehai.
Bakteria wa Mycobacterium Tuberculosis (TB) anaweza kushambulia sehemu yoyote ya mwili, lakini mara nyingi hushambulia mapafu.
TB (1)Mtu anaweza kuwa na kifua kikuu kikali au tulivu. Kifua kikuu kikali au ugonjwa wa TB inamaanisha kuwa bakteria wanashambulia mwili na mfumo wa kinga unashindwa kuwazuia wasisababishe ugonjwa. 

Watu wenye kifua kikuu kikali kwenye mapafu yao wanaweza kuambukiza bakteria mtu mwingine yeyote anayekuwa karibu yake kwani anapokohoa, kupiga chafya au kutema mate, mtu aliyekaribu anaweza kuwavuta bakteria wa kifua kikuu wakati wa kupumua na kuambukizwa. 

Watu wanaweza kuambukizwa bakteria wa kifua kikuu pia wasiokuwa wakali mwilini mwao. Iwapo mtu ana kifua kikuu tulivu, ina maana kuwa mwili wake umefanikiwa kupambana na bakteria wa maradhi hayo kikamilifu na kuwazuia wasisababishe ugonjwa. 

Watu wenye kifua kikuu tulivu hawajisikii wagonjwa, hawana dalili, na hawawezi kuwaambukiza wengine.
Pata dondoo za afya za madaktari bingwa kwenye simu yako ya Vodacom bure: Tuma DAKTARI kwenda 15542

USIPITWE! JIUNGE NASI FACEBOOK

Subscribe to this Blog via Email :

TOA MAONI YAKO HAPA (MATUSI HAYARUHUSIWI)

Note: Only a member of this blog may post a comment.