Sunday, August 2, 2015

Anonymous

DONDOO MUHIMU Kelekea Pambano KALI leo la ARSENAL vs CHELSEA

arsenal-vs-chelsea
MABINGWA wa Kombe la FA, Arsenal leo wanajitupa uwanjani kukwaana na mabingwa wa Ligi Kuu ya England, Chelsea kwenye mechi ya Ngao ya Jamii.
Mechi hiyo ya leo itapigwa kwenye Uwanja wa Wembley ikiwa ni maalum kwa ajli ya kufungua msimu mpya wa Ligi Kuu ya England.
ars vs chels
Pambano la leo limekuwa gumzo kubwa miongoni mwa mashabiki wa soka kutokana na mambo mengi ikiwemo suala la uhasama wa makocha wa timu hizo Arsene Wenger na Jose Mourinho ambao wamekuwa wakiupiana vijembe kila kukicha.
Wenger hajawahi kuifunga Chelsea ikiwa chini ya Mourinho kwa hiyo mashabiki wanasubiri kwa hamu mpambano wa leo kuona kama historia hiyo itavunjwa.

USIPITWE! JIUNGE NASI FACEBOOK

Subscribe to this Blog via Email :

TOA MAONI YAKO HAPA (MATUSI HAYARUHUSIWI)

Note: Only a member of this blog may post a comment.