Rapper Bonge la Nyau atafurahi zaidi kama utamuita jina lake jipya, Nyauloso.
Bonge la Nyau amedai kuwa sababu za kutaka kubadilisha jina hilo ni
kutokana na kupewa ushauri na watu wengi wanaodhani jina lake lina
tafsiri hasi kwenye masikio ya baadhi ya mashabiki wake.
“Watu wengi wamekuwa wakiongea kwamba Bonge la Nyau halisound vizuri,
kwa kipindi hiki ambacho nimetoa Vice Versa, watu wamependa sana
Nyauloso,” rapper huyo ameiambia Bongo5.
“Kwahiyo mimi hapa nimeongeza
ili kuwa na option kama mtu hatolipenda Bonge la Nyau kwasababu kuna
watu walishalizoea hivyo Nyauloso nitakuwa nalitumia kama nickname na
najua watu wengi pia wanalipenda,” ameongeza.
Amedai kuwa Nyauloso ni jina alilopewa na rafiki yake wa kike.
Kwa upande wa jina la Bonge la Nyau, Nyauloso amedai kuwa jina hilo
alipewa na msichana waliyesoma wote O-Level kwenye shule ya Benjamin
Mkapa ambapo rapper Shetta alikuwa classmate wake.
“Kuna dada mmoja alikuwa amenizidi madarasa aliniita ‘Big Cat’,”
amesema Nyauloso. “Aliniambia napenda unavyofanya nataka nikuite big
cat. Msichana huyo alimwambia jina hilo kwa Marekani hupewa watu
wanaofanya mambo makubwa. Nyauloso anasema jina hilo alikuja kuanza
kulitumia rasmi alipoanza muziki serious na kuamua kulibadilisha kuwa
Kiswahili.
-via bongo5

Note: Only a member of this blog may post a comment.