Tuesday, August 25, 2015

Anonymous

Bonge la Nyau sasa anapenda umuite ‘Nyauloso’, aeleza sababu za kutaka kubadili jina!

Rapper Bonge la Nyau atafurahi zaidi kama utamuita jina lake jipya, Nyauloso.
925590_932946110077873_1568089206_n
Bonge la Nyau amedai kuwa sababu za kutaka kubadilisha jina hilo ni kutokana na kupewa ushauri na watu wengi wanaodhani jina lake lina tafsiri hasi kwenye masikio ya baadhi ya mashabiki wake.
“Watu wengi wamekuwa wakiongea kwamba Bonge la Nyau halisound vizuri, kwa kipindi hiki ambacho nimetoa Vice Versa, watu wamependa sana Nyauloso,” rapper huyo ameiambia Bongo5.

“Kwahiyo mimi hapa nimeongeza ili kuwa na option kama mtu hatolipenda Bonge la Nyau kwasababu kuna watu walishalizoea hivyo Nyauloso nitakuwa nalitumia kama nickname na najua watu wengi pia wanalipenda,” ameongeza. 

Amedai kuwa Nyauloso ni jina alilopewa na rafiki yake wa kike.
Kwa upande wa jina la Bonge la Nyau, Nyauloso amedai kuwa jina hilo alipewa na msichana waliyesoma wote O-Level kwenye shule ya Benjamin Mkapa ambapo rapper Shetta alikuwa classmate wake. 

“Kuna dada mmoja alikuwa amenizidi madarasa aliniita ‘Big Cat’,” amesema Nyauloso. “Aliniambia napenda unavyofanya nataka nikuite big cat. Msichana huyo alimwambia jina hilo kwa Marekani hupewa watu wanaofanya mambo makubwa. Nyauloso anasema jina hilo alikuja kuanza kulitumia rasmi alipoanza muziki serious na kuamua kulibadilisha kuwa Kiswahili.
-via bongo5

USIPITWE! JIUNGE NASI FACEBOOK

Subscribe to this Blog via Email :

TOA MAONI YAKO HAPA (MATUSI HAYARUHUSIWI)

Note: Only a member of this blog may post a comment.