Mayasa Maliwata
STAA wa filamu Bongo, Lucy Komba ameamua
kumpa makavu laivu msanii asiyeishiwa vioja, Fatuma Ayubu `Bozi’
anayetajwa kuwa na orodha kubwa ya mastaa aliobanjuka nao kwa kumtaka
akumbuke kutumia kinga ama kutulia na bwana mmoja.
Akibonga na paparazi wetu kwa njia ya
simu akiwa nchini Denmark, Lucy alisema anamshangaa sana msanii huyo
kutokana na tabia yake ya kupenda kubanjuka ovyo na wasanii wenzake bila
kujua kuwa ulimwengu wa sasa umeoza.
“Siyo siri huyu msanii ananikera sana
isitoshe anatudhalilisha, sioni faida yoyote anayoipata zaidi ya
kuhatarisha maisha yake, ni vyema angetulia na mmoja na kama hawezi basi
kiukweli akumbuke kutumia kinga laa sivyo yatamkuta makubwa,” alisema
Lucy.

Note: Only a member of this blog may post a comment.