WIZKID ATENGULIWA UBALOZI MTN!
Lagos, Nigeria
MKALI
wa AfroPop kutoka nchini Nigeria, Ayodeji Balogun ‘Wizkid’ametenguliwa
kuendelea kuwa Balozi wa Kampuni la MTN kama alivyokuwa hapo mwanzo.
Kwa
mujibu wa vyanzo vya karibu kutoka kampuni hiyo inayohusika na
mawasiliano, inadaiwa kuwa Wizkid amesitishwa kuendelea kuwa balozi
baada ya kuonekana kuwa hana faida, wakati msanii Wizkid akitenguliwa
ubalozi wenzake Davido, Don Jazzy,Tiwa Savage na Iyanya wakipewa
mikataba mipya.
“Kuna wasanii wengi sana wanaofanya vizuri nchini Nigeria tunawaomba
waendelee kuweka kazi zao katika mitandao ya muziki muda ukifika
tukiwahitaji tutawachukua,” alisema Iweanoge, msemaji wa MTN.
USIPITWE! JIUNGE NASI FACEBOOK
TOA MAONI YAKO HAPA (MATUSI HAYARUHUSIWI)
Note: Only a member of this blog may post a comment.