Gabriel Ng’osha
Kivipi? Taarifa ikufikie kuwa komediani maarufu Bongo, Steven Mengere
‘Steve Nyerere’ amefunguka kuwa yeye na staa wa sinema za Kibongo,
Wastara Juma ni damdam.
Steve alisema hayo wikiendi iliyopita wakati akichukua fomu ya
kugombea nafasi ya ubunge katika Jimbo la Kinondoni, Dar kwa leseni ya
Chama Cha Mapinduzi (CCM).
“Mimi na Wastara ni damdam katika kuhakikisha tunashinda
kinyang’anyiro cha ubunge hapo Oktoba. Mimi nagombea Jimbo la Kinondoni
na mwenzangu anawania viti maalum Morogoro,” alisema Steve.

Note: Only a member of this blog may post a comment.